Saturday, 19 October 2013

Ijue Sababu ya ,Fid Q, Ay, Witnesz, na F.A kupeana madili ya nje ya nchi.

       

Fid Q kushoto, Ay kulia akifuatiwa na Witnesz Tz ama the fitnes pamoja na Mwana Falsafa kulia

FID Q                                                                                                  AY
         


WITNESZ                                                                  MWANA F.A

Ijue sababu ya wasanii wengi wa bongo kulalamika juu ya ,fid Q, Ay, Witnesz, na F.A kupeana madili ya nje ya nchi,
sababu kubwa si kupeana kama wanavyodai raia wengi suala ni kwamba wasanii wengi ni wavivu na si wachangamkia dili na hawako sharp wanajivuta mno,nitakupa mifano miwili;

Mfano A; 

     Kuna wakati niliwahi kutangaza kwa njia ya redio jamani kama kuna wasanii wowote wale, ambao wangependa kujua ni namna gani anaweza kupeleka video zake chanel o,anaweza nitafuta au anicheki hewani nitamuelekeza, alinicheki msanii mmoja tu jina (kapuni) naye pia baada ya kumuelekeza alitaka nikamchukulie fomu nimpelekee, japo mwingine ambaye alifanikiwa kutuma kwa kupitia ujmbe kama huo ni Black rhino (black chattah) na kufanikiwa kwenda kwenye tuzo za chanel o music video awards'
       Na nilitangaza hivyo kwa kuwa roho iliniuma sana baada ya kuona wanigeria wakiwa na ushirikiano hatari tupu na kufurika kwenye tuzo hizo na sisi wa Tanzania tukichanganyika na Africa mashariki kiujumla labda ndo tunaweza fua dafu kidogo kama yaliyomo ama utangulizi kabla ya kusoma kitabu, na hawaishii kushirikiana tu kwa kupeleka kazi nyingi nzuri,ila kwa kuwa muziki na mavazi ni pete na kidole cha ndoa, na wanamitindo wao hawapo nyuma kwenye kuwavalisha wasanii wao hao si kwenye red carpet ama music videos.
   Ambapo huwa mara nyingi ndo designers wengi huwa wanatambulika kwa faida zao wenyewe kwa kupitia mfumo huu,na niliporudi nika muapproach moja ya wanamitindo wetu nikidhani nitasaidia si kupeperusha tu bendera ya Tanzania kwa kutumia kipaji changu bali hata kuwasilisha sanaa hiyo ya wanamitindo wetu wa bongo,mambo yalienda ndivyo sivyo,kiufupi nilivunjika moyo sana tu baada ya kuambiwa nitoe pesa ya material Dah! nguo nitakazo zitangaza zake,jina nitakalo litangaza lake kwenye red carpet hizo kwa kumnadi na bado anataka nimpatie pesa za material, na endapo wangejua ya kuwa video zetu za muziki ni njia moja wapo kubwa madesigner wengi wanajulikana duniani kupitia mfumo wa kuzidhamini video za muziki na filamu na huwa wanawafuata wenyewe artist wanaodhani watawawezesha na wanaofanya vizuri kama njia moja wapo ya kutangaza na kujiongeza katika biashara yao hiyo ya ubunifu wa mavazi ninaishia hapa kama ni mwanamitindo wa bora elewa na kama bora mwanamitindo ishia hivyo hivyo na kutegea pesa za material!

   Mfano;B
Nilikuwa ninaenda tena kwenye tuzo za chanel o mjini afrika kusini kuna jamaa yangu mmoja yeye ni mganda amefungua kituo cha redio kwa njia ya mtandao aitwae kaunda ,aliniomba nimpelekee nyimbo za wabongo amefungua kituo hicho ajiri ya kupiga nyimbo za afrika mashariki zaidi kama kawaida yangu ya kutokata tamaa nikatangaza redioni usiku asubuhi yake tu AY alikuwa ni wa kwanza kuniletea cd yenye audio zake, na wasanii wengine waliahidi kuniletea mpaka nikaondoka,na sikuwaona tena, je tunapendeleana kweli ama tunajua tunachotaka na kuthamini tulicho nachona biashara yetu kiujumla??
   Hii ni sawa sawa na kuogopa kuingia supermarket wabongo wengi wanatabia hiyo, kwa kuogopa bei kuwa ni kubwa kisa kiyoyozi lakini kiuharisia supermarket ni masoko ambayo yenye usafi wa hali ya juu na yenye bidhaa zilizokaa kwenye mpangilio mzuri na hakuna kupunguziana bei lakini kuna vitu vingine ni bei chini sana na wakati mwingine kila supermarket huwa ina vitu vyake vya bei ghali na ya bei ya chini na kila supermarket ina sifa yake kama sokoni kariakoo,mwananyamala manzese, ilala N.k

    Sasa kwa mara nyingine tena kuna jamaa wanatoka Uganda wanaitwa BADI FLMs wanakuja toka Uganda kufanya video yangu mpya jina (kapuni) audio yake itaanza toka next week, nimekwisha pigia simu wasanii kibao wanazunguka mbuyu na ninaandika kwa njia ya mtandao tena labda wapo wenye nia ya kujiongeza na sijaweza wafikia kiukweli hawa jamaa wanawanavideo kali hadi quality yao pia ni nzuri wamefanya video ya ngama kama valu valu ya Chameleone na kadha wa kadha zikiwemo za Blue three ukitaka kuwajua zaidi video walizofanya nyingi za akina Radio na Weasle kwa yeyote atakaye hitaji kufanya video na hawa jamaa anaweza dandia lifti msiogope bei nimechonga nao watafanya bei za kawaida ila wanakuja tarehe 26 /10 na hawakai sana, kazi kwenu mie ninapatikana kwa nambari 0753 32 00 09 /0715 700014 hii ni kwa mwenye nia ya kujiongeza na biashara yake burudani! muwe na amani!

3 comments:

  1. Unafanya vyema sana Witness, Lakini naamini unamoyo wa kiujasiliamali
    Sifa mojawapo ya mjasiliamali ni kutokata Tamaa, maanayake ni kwamba nakupa moyo uendelee kuwahimiza kwasababu ili mabadiliko yatokee, anapaswa mmoja amwage damu kwaajiri ya wengi... mimi binafsi naamini wewe utaumia kwaajiri ya wengi na jina lako litakumbukwa

    ReplyDelete
  2. Thanks silvanus I highly apreciate it!

    ReplyDelete
  3. Good stuff witness, congrats and keep on keeping on lady!

    ReplyDelete